Jumapili, 23 Julai 2017

IRINGA YAPEWA MIL 300 KWA ELIMU MAALUMU



Na. Mwandishi Maalum, Iringa
Serikali imejipanga kukabiliana na changamoto za elimu maalum kwa shule za msingi na sekondari mkoani Iringa kwa kuanza imepeleka shilingi milioni 300 ili kuwawezesha watoto kusoma katika mazingira mazuri na rafiki.

Kauli hiyo ilitolewa na waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Joyce Ndalichako alipotembelea shule ya msingi Mtwivila iliyopo katika Manispaa ya Iringa juzi.

Prof. Ndalichako alisema kuwa elimu maalumu nchini inakabiliwa na changamoto nyingi ambazo wizara yake haiwezi kuzimaliza kwa siku moja. Alisema kuwa katika kukabiliana na changamoto hizo, wizara yake ilipeleka mkoani Iringa shilingi milioni 300 kwa ajili ya shule za msingi na sekondari zenye mahitaji maalumu.

Akiongelea changamoto ya fedha za nauli kwa watoto wa shule ya msingi Mtwivila yenye watoto wenye mahitaji maalum pindi shule inapofungwa, Prof. Ndalichako aliwataka wazazi kuwapa kipaombele watoto hao kwa kuwapatia nauli ili waweze kurudi nyumbani shule zinapofungwa. 

Aidha, alitatoa wito kwa jamii kununua bidhaa zinazotengenezwa na watoto wanaosoma elimu maalumu kama njia ya kuunga mkono juhudi zao.

Akishukuru kwa ziara ya waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mkuu wa mkoa wa Iringa Amina Masenza alisema kuwa ziara hiyo imewajengea uwezo watoto wenye mahitaji maalumu na kujiamini zaidi katika masomo yao. 

Aidha, alimtaka Katibu Tawala mkoa wa Iringa kusimamia vifaa vyote vilivyotolewa na wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kwa ajili ya wanafunzi wenye mahitaji maalumu ili viweze kuwanufaisha watoto wote mkoani Iringa. 
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...