Jumanne, 15 Agosti 2017

KUU IRINGA KUONGOZA OPERESHENI NYALUU



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Iringa kuongoza operesheni ya kuwaondoa wakulima katika bonde la Nyaluu katika kudhibiti ujangili katika hifadhi ya Taifa ya Ruaha.

Kauli hiyo ilitolewa na mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Iringa, Amina Masenza katika kuhitimisha ziara ya waziri wa maliasili na utalii wilayani Iringa jana.

Masenza ambaye pia ni mkuu wa mkoa wa Iringa alisema kuwa shughuli zote za kibinadamu ndani ya eneo la Nyaluu haziruhusiwi na eneo hilo lihifadhiwe. Aidha, alishauri kambi ya doria ijengwe katika eneo hilo ili kurahisisha udhibiti wa ujangili katika hifadhi ya Taifa ya Ruaha na eneo hilo ambalo ni mapito ya wanyama na eneo la jumuiya ya hifadhi ya wanyamapori Pawaga na Idodi (Mbomipa) kwa ujumla.

Aidha, aliitaka halmashauri ya wilaya ya Iringa kuorodhesha wakulima wote wanaolima katika bonde la Nyaluu na kuwaandikia barua ya zuio la kulima eneo hilo.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...