Jumatatu, 7 Agosti 2017

WAKULIMA WATAKIWA KUTUNZA KUMBUKUMBU


Na. Dennis Gondwe, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa
 
Wakulima na wajasiriamali watakiwa kuweka utaratibu wa kutunza kumbukumbu za mahesabu ili kubaini faida na hasara inayopatikana katika shughuli zao.

Kauli hiyo ilitolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Iringa, Wamoja Ayubu alipokuwa akifanya majumuisho ya ziara ya kukagua mabanda alipomuwakilisha mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza.

Ayubu alisema “ni vizuri wakulima na wajasiriamali wakafundishwa jinsi ya kutunza kumbukumbu za mahesabu ya kilimo na uzalishaji ili kufahamu gharama na mwenendo mzima wa kazi wanazofanya. Kufanya hivyo kutamsaidia mkulima na mjasiriamali kujua hali halisi ya kazi anayofanya na kuwawezesha kutoa ushuhuda”. 

Katibu Tawala Mkoa wa Iringa aliwataka wakurugenzi kuhakikisha wanawapangia malengo maafisa ugani ili waweze kutoa tija katika shughuli za kilimo na mifugo. 

Hakikisheni wataalam hawa mnawapangia malengo yanayopimika na wawe na mpango kazi unaotekelezeka. Utaratibu huu utawawezesha wakulima na wafugaji kuhudumiwa” alisisitiza Ayubu.

Akiongelea uzalishaji katika mashamba ya kuzalisha mitamba ya serikali ya Kitulo na Sao-Hill, Katibu Tawala Mkoa aliyatka mashamba hayo kuongeza uzalishaji wa mitamba ili kukidhi mahitaji ya mitamba katika mikoa ya nyanda za kuu kusini. 

Mahitaji ya mitamba ni makubwa kwa mikoa ya nyanda za juu kusini, hivyo soko ni la uhakika. Kinachotakiwa ni kuzalisha mitamba zaidi” alisisitiza Ayubu. 

Aidha, aliyakata mashamba hayo kuongeza matumizi ya teknolojia katika uzalishaja wa mitamba.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...