Jumapili, 28 Januari 2018

RC MASENZA AFURAHISHWA URITHISHAJI WATOTO MBINU ZA UFUGAJI



Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza amefurahishwa na utaratibu wa kurithisha mbinu za ufugaja kwa wanafunzi kwa lengo la kuwajengea moyo wa kuwajibika wanafunzi wanufaika wa mpango wa TASAF wilayani Mufindi.

Masenza alisema hayo alipokuwa akiongea na wanufaika wa mpango wa kunusuru kaya masikini na wanafunzi wanaonufaika na fedha za elimu kupitia TASAF katika shule ya msingi Mafinga iliyopo mjini Mafinga jana.

Masenza alisema kuwa utaratibu wa kuwafundisha watoto wadogo ufugaji wa mifugo wadogo kama kuku ni jambo zuri. Alisema kuwa utaratibu huo unawaandaa watoto hao kuweza kujitegea wanapokuwa na kuondoa utegemezi kwa jamii inayowazunguka. Aidha, alitoa wito kwa wanufaika wengine wa mpango wa TASAF na jamii kwa ujumla kuiga utaratibu huo.

Awali mwanafunzi mnufaika wa shule ya msingi Mafinga, Hosana Chaula aliishukuru serikali kwa kuanzisha mpango wa kunusuru kaya masikini. Alisema kupitia mpango huo ameweza kununuliwa vifaa na sare za shule. 

Pia nilinunuliwa kuku 4 nikawahudumia na wakatotoa vifaranga 10. Kati ya vifaranga hivyo, vifaranga vitano vilikufa” alisema Chaula.
=30=

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...