Alhamisi, 27 Machi 2014

TAARIFA YA MAJI MKAO WA IRINGA ILIYOSOMWA KATIKA MAADHIMISHO YA WIKI YA MAJI KIMKOA TAREHE 17-22 MACHI, 2014



 1.0      UTANGULIZI
Ndugu. Mgeni rasmi, 
Katibu Tawala wa Mkoa. Mkoa wa Iringa unaadhimisha wiki ya maji kwa mara ya 26, tangu maadhimisho haya yalipoanza kuadhimishwa hapa nchi kwa mara ya kwanza mwaka 1988. Maadhimisho haya yaliongezwa nguvu na umuhimu na Azimio Na. 47/193 la 22 Desemba, 1992 la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. 

Wiki ya maji huunganisha wadau wa Sekta mbalimbali katika kutathimini na kupanga jinsi ya kuboresha upatikanaji na utumiaji wa rasilimali za maji kwa manufaa ya wote. Mkoa wa Iringa unaungana na Watanzania wote katika maadhisho ya wiki ya maji ya mwaka huu yenye kaulimbiu isemayo ‘Uhakika wa Upatikanaji Maji na Nishati’

Nanukuu
‘By the resolution 47/193 of 22 December 1992, the General Assembly declared 22 March of each year World Day to remind everybody that concrete efforts to provide clean drinking water and increase awareness world-wide of the problems and of the solutions, can help make the difference. DO YOUR PART. PLEASE USE WATER WITH CARE. REMEMBER THOSE PLACES WITH NO WATER OR POOR WATER QUALITY’.

Ndugu Mgeni Rasmi
Maadhimisho haya ni ya 26 na hufanyika kila mwaka kuanzia tarehe 16 hadi 22 mwezi Machi.  Maadhimisho ya mwaka huu yanafanyika Kitaifa Mjini Dodoma. Aidha, Kimkoa yanafanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo na hususan yanazinduliwa katika kijiji cha Ihimbo. 

Ndugu Mgeni Rasmi.
Kaulimbiu ya wiki ya maji ya mwaka huu inatukumbusha jinsi ambavyo uhusiano wa upatikanaji wa huduma ya maji unavyotegemeana na upatikanaji wa huduma ya nishati, hususan nishati ya umeme (hydro power). Hivyo, kuboresha kitu kimoja ni kuboresha vitu vyote viwili.

2.0 HUDUMA YA MAJISAFI
2.1  Maji Mijini
Wananchi wanaopata huduma ya majisafi Mijini katika Mkoa wa Iringa 189,644 kati ya wananchi 247,156 ambao ni sawa na asilimia 76.7 ya wanchi waishio mijini. Hali ya huduma ya maji Mijini inategemewa kuongezeka mara baada ya kutekelezwa kwa miradi katika miji ya Ilula, Kilolo na Mafinga. Miradi hii inategemewa kutekelezwa kupitia program ya Maendeleo ya Sekta ya Maji (WSDP) ambapo jumla ya wananchi 57,512 watapata huduma bora ya majisafi na salama.

3.0  Hali ya Upatikanaji wa Huduma ya Maji Vijijini

Jumla ya wananchi wapatao 441,170 sawa na 63.6 % ya wananchi wote waishio vijijini wanapata huduma ya maji safi na salama kupitia miradi iliyojengwa kwa kutumia teknolojia mbalimbali zikiwemo:- visima virefu na vifupi, maji ya bomba na visima vya asili na chemichemi zilizo boreshwa. Upatikanaji wa huduma ya maji kwa upande wa vijijini kwa kila wilaya ni kama ifuatavyo: -
i)        Halmashauri ya Manispaa ya Iringa (vijijini - peri urban) inatoa huduma ya maji kwa wananchi wapatao 8,668, sawa na asilimia 76.2 
ii)      Halmashauri ya Wilaya ya Iringa inatoa huduma ya maji kwa wananchi wapatao 172,742, sawa na asilimia 68.0 
iii)    Halmashauri ya Wilaya ya Kilolo inatoa huduma ya maji kwa wananchi wapatao 94,288, sawa na asilimia 57.9 
iv)    Halmashauri ya Wilaya ya Mufindi inatoa huduma ya maji kwa wananchi wapatao 159,763, sawa na asilimia 60.1 
Utoaji wa huduma unatarajia kuongezeka mara baada ya kukamilika kwa ujenzi wa miradi ya maji katika vijiji kumi kwa kila Halmashauri.

 4.0  Ujenzi wa miradi ya matokeo makubwa sasa (BRN)
Ndugu Mgeni Rasmi.
Mkoa unajenga miradi 42 ya maji yenye kuleta matokeo makubwa sasa. Miradi hiyo iko katika hatua mbalimbali ya ujenzi, aidha mkoa unahitaji kiasi cha Tshs. Bilioni 11.582 kwa ajili ya kuwalipa Makandarasi, Wataalam Waelekezi na usimamizi na ufuatiliaji wa ujenzi wa miradi hiyo. 

5.0  Wadau wa Maji
Ndugu Mgeni rasmi.
Mkoa unasharikiana vizuri na wadau mbalimbali katika ujenzi na utoaji wa huduma ya maji na usafi wa mazingira, wadau hao ni pamoja na Living Water International, Rural Development Organization, Kanisa la RC, St. Paul Partners, MLFM and AVSI, IDYDC kupitia program ya MAUWA, Emmanuel International na UNICEF  

6.0  Mifuko ya maji
Ili kuwa na miradi endelevu uundaji wa kamati za maji na vyombo imara vya watumiamaji ni jambo la msingi. Kwa mantiki hiyo Mkoa una jumla ya kamati za maji ni 162, mifuko ya maji 143 na vyombo vya watumia maji 10.

7.0  Hali ya Watumishi wa Kada za Maji
Mkoa una jumla ya watumishi 64 wa kada za maji, wakiwemo Wahandisi, Mafundi sanifu na Mafundi sanifu wasaidizi. Kwa ujumla Mkoa unaupungufu wa wataalam wa kada za maji 31.

Ndugu Mgeni Rasmi

8.0  Changamoto Mbalimbali Zinazoikabili Sekta ya Maji Huduma ya Maji na usafi wa Mazingira     

    i.        Wananchi kutochangia kikamilifu mifuko ya maji vijijini kutokana na uelewa mdogo wa sera ya maji ya mwaka 2002.
   ii.        Wananchi kutotunza miradi ya maji mara baada ya miradi kukamilika na kukabidhiwa kwa wananchi
 iii.        Wananchi kuharibu vyanzo vya maji kwa kufanya shughuli za kibinadamu ndani ya maeneo ya vyanzo vya maji.
 iv.        Uchakavu wa miundombinu ya maji hasa miradi wa Ilula na Isimani.
  v.        Kuchelewa kupata fedha za matumizi mengineyo au kutengewa kiasi kidogo cha fedhakisicholingana na mahitaji halisi.
 vi.        Kupanda kwa gharama za umeme wa kuendeshea mitambo ya kusukuma maji katika mji wa Mafinga na mamlaka ya maji ya IRUWASA
vii.        Uchache wa fedha kwa ajili ya ujenzi, ukarabati na upanuzi mkubwa wa miradi ya zamani kama miradi ya Mbalamaziwa na Malangali, Isimani na Ilula

9.0  Mikakati ya Mkoa ya Kukabiliana na Changamoto Zilizopo

    i.        Kuandaa mpango wa uvunaji wa maji ya mvua na kuatafua fedha kwa ajili ya utekelezaji wake.
   ii.        Idara za maji za kila Halmashauri zinaendelea kutoa elimu kwa Wananchi kuhusu uundaji na Usajiri wa Jumuiya za watumiamaji, ufunguaji wa mifuko ya maji uendeshaji na utunzaji wa miradi ya maji mijini na vijijini kwa mujibu wa sheria ya maji Na. 11 na 12 ya mwaka 2009 na Sera ya maji ya mwaka 2002.

Mwisho
Ndugu Mgeni Rasmi
Tunayo furaha kubwa kukubali mwaliko wetu na kushiriki kwako katika uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya maji Kimkoa yanayofanyika leo tarehe 17 Machi, 2014 katika kijiji cha Ilamba, Halmahsuri ya wilaya ya Kilolo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Habari zinazoendelea hivi sasa

SERIKALI KUWEZESHA VIJANA KUKOPA

Na. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Iringa Serikali itaendelea kuwawezesha vijana kwa kuwatengenezea mazingira mazuri ya mikopo ili waweze k...